NILIOLEWA NA KAKA YANGU SEHEMU YA PILI.....
'Mungu chukua uhai wangu..chukua uhai wangu nimechoka kuishi mateso ya dunia'
Baba alimsogelea mama huku mkono wake wa kulia umeshika mkanda wa suruali yake. Mama akiwa uchi wa mnyama, amejikunja chini kwa uoga kama kifaranga. Mama Hamis naye amekaba shingo yangu; kunizuia nisiokoe maisha ya mama yangu. Mdogo wangu Shadrack yupo pembeni ya mama analia kama yatima. Bila huruma, bila kujali baba aliinua mkono wake wenye mkanda na kuanza kumsulubu mama mbele ya macho yetu. Mbele ya hawala yake.