MAISHA YANGU DUNIANI.
"Mahojiano kati ya Mimi na Mungu"
Simulizi ya uamsho.
Kabla sijaondoka duniani niliishi maisha ya bora liende. Nilitumika na watu wenye ndoto kubwa kama spea ya trekta. Dini yangu, nilijivunia dini yangu na kupumbazika kwa majivuno. Wale waliotofautiana na mimi; niliwatenga na kuwahukumu kama Mungu. Sikujua ukweli. Sikujua kuwa yote niliyosoma. Yote yaliyokuwa kichwani mwangu yalikuwa ni upupu tu. Yaliniendesha na kunifanya niishi kama mashine isiyo na roho kwa ndani. Nilijikuta miaka yangu inakimbia tu; hakuna cha maana nilichofanya duniani.



