Swahili quotes

Tuesday, July 1, 2014

Nikumbuke Mpenzi wangu sehemu ya tatu...

 NIKUMBUKE MPENZI WANGU...REMEMBER ME MY LOVE SEHEMU YA TATU

"narudia tena hampaswi kujua chochote kwa undani kuhusu huyu Dada"
Maneno ya dokta Adam yalizidi kunichanganya. Labda amechanganyikiwa. Kuna nini kinaendelea katika maisha yangu? Nimetokewa na nini? Ni nani amehusika katika ajari yangu? Ndugu zangu wako wapi? mume Wangu Osward yuko wapi? Baada ya maongezi yao'; Dokta Adam aliondoka na kuniacha mpweke tena. Walibaki wahudumu wawili Deborah na Frank na Dokta Michael. Baada ya dakika kadhaa nikasikia sauti ya Michael;
 "hakuna MTU yeyote aliyekuja kumuulizia mgonjwa huyu?"  Deborah akajibu "yaani huyu Dada toka aletwe hapa hospitali ni Dokta Adam pekee amekuwa akimhudumia kisiri. Na zaidi; tumeambiwa harusiwi mtu yeyote kuja kumuona wala kujua uwepo wake; hasa ndugu zake"