Swahili quotes

Tuesday, July 1, 2014

Nikumbuke Mpenzi wangu sehemu ya tatu...

 NIKUMBUKE MPENZI WANGU...REMEMBER ME MY LOVE SEHEMU YA TATU

"narudia tena hampaswi kujua chochote kwa undani kuhusu huyu Dada"
Maneno ya dokta Adam yalizidi kunichanganya. Labda amechanganyikiwa. Kuna nini kinaendelea katika maisha yangu? Nimetokewa na nini? Ni nani amehusika katika ajari yangu? Ndugu zangu wako wapi? mume Wangu Osward yuko wapi? Baada ya maongezi yao'; Dokta Adam aliondoka na kuniacha mpweke tena. Walibaki wahudumu wawili Deborah na Frank na Dokta Michael. Baada ya dakika kadhaa nikasikia sauti ya Michael;
 "hakuna MTU yeyote aliyekuja kumuulizia mgonjwa huyu?"  Deborah akajibu "yaani huyu Dada toka aletwe hapa hospitali ni Dokta Adam pekee amekuwa akimhudumia kisiri. Na zaidi; tumeambiwa harusiwi mtu yeyote kuja kumuona wala kujua uwepo wake; hasa ndugu zake"

Sunday, June 29, 2014

Naijutia Ndoa Yangu Sehemu ya pili

Mama yangu mzazi Eugenia Mwafilombe na baba yangu wa kambo Patrick Sichalwe hawakutoa kitu. Hata zawadi ya pipi; iliniuma sana. Lakini nilimshukuru Mungu kuwa siku ya harusi walifunga midomo yao; hawakutoa siri ya yote niliyofanya ili niolewe na Benson. 

STOLEN DESTINY PART 1


“When all people you love and care, turn against your inner voice.  They push you to hell, and your destiny is stolen. Now you are back with no love, no life in you, but desire to turn the world upside down”

  STOLEN DESTINY PART 1



Life is a journey; and the roads we travel have twisted turns; which sometime lead us to unexpected places, and to unexpected people. I met this guy; who then with only one night he destroyed my life forever. It’s the night that my stress pushed me into hell. The night with no stars, no hope and no life in me.

Saturday, June 28, 2014

THE FAKE PRESIDENT/Rais Feki sehemu ya 1

Mtu yeyote anaweza kukua, kujifunza na kuwa Rais. Lakini, si kila Rais anaweza kufanya, kusababisha mabadiliko na mapinduzi makubwa kiuchumi,kijamii na kisiasa. Kiti cha Urais; ni kwaajili ya mtu maalumu mwenye tabia iliyotukuka na mtu wa watu, tabia kubwa,mgumu, mwenye uwezo mkubwa kiakili, maono makubwa, msimamo mkali,mzalendo na mwenye njaa ya mabadiliko asiyeendeshwa na watu wala matukio. Ni kwa mara ya kwanza Tanzania inampata Rais mwenye uwezo mkubwa uliotukuka. Mwenye maono makubwa . Mwenye hekima. Mwenye upendo wa dhati. Mzalendo wa kweli. Jasiri. Mtu wa watu.  Mh. Kennedy P. Kyando; rais mpya aliyeshinda kwa kishindo kupitia chama cha upinzani kiichwacho people's welfare party(pWp).

Friday, June 27, 2014

MAISHA YANGU DUNIANI SEHEMU YA PILI

MAISHA YANGU DUNIANI. 
"Mahojiano kati ya Mimi na Mungu"
Simulizi ya uamsho. 
Kabla sijaondoka duniani niliishi maisha ya bora liende. Nilitumika na watu wenye ndoto kubwa kama spea ya trekta. Dini yangu, nilijivunia dini yangu na kupumbazika kwa majivuno. Wale waliotofautiana na mimi; niliwatenga na kuwahukumu kama Mungu. Sikujua ukweli. Sikujua kuwa yote niliyosoma. Yote yaliyokuwa kichwani mwangu yalikuwa ni upupu tu. Yaliniendesha na kunifanya niishi kama mashine isiyo na roho kwa ndani. Nilijikuta miaka yangu inakimbia tu; hakuna cha maana nilichofanya duniani.

Thursday, June 26, 2014

SIRI INAYOANGAMIZA SEHEMU YA PILI.


SIRI INAYOANGAMIZA SEHEMU YA PILI.


"Beee mama" Helena aliitika na kumwacha Steve bado ameduwaaa chumbani kwake. Alipofika sebuleni alikuta mama yake amesimama, mkono wake wa kulia umeshikilia kitambaa cha kusafishia vyombo.
"Steve anafanya nini chumbani kwako?" Mama aliuliza. 
"aah! alikuwa anauliza kama kuna rafiki yangu yeyote alikuja jana"

Wednesday, June 25, 2014

NAIJUTIA NDOA YANGU...SEHEMU YA KWANZA

 
Ilikuwa kama ndoto kuolewa na mtoto wa waziri mkuu. Benson Mkama. Siku ya harusi ilikuwa ni balaa. Nilikuwa na furaha  isiyo kifani. Nilijua kuwa umaskini sasa basi. Padri akasema 
"Benson Mkama, unamkubali Jackline Stephano kuwa mke wako, katika shida na raha; katika hali zote mpaka kifo kitakapowatenganisha?"