Swahili quotes

Wednesday, June 25, 2014

NAIJUTIA NDOA YANGU...SEHEMU YA KWANZA

 
Ilikuwa kama ndoto kuolewa na mtoto wa waziri mkuu. Benson Mkama. Siku ya harusi ilikuwa ni balaa. Nilikuwa na furaha  isiyo kifani. Nilijua kuwa umaskini sasa basi. Padri akasema 
"Benson Mkama, unamkubali Jackline Stephano kuwa mke wako, katika shida na raha; katika hali zote mpaka kifo kitakapowatenganisha?"

Niliolewa na kaka yangu sehemu ya 2

 NILIOLEWA NA KAKA YANGU SEHEMU YA PILI.....

'Mungu chukua uhai wangu..chukua uhai wangu nimechoka kuishi mateso ya dunia'
Baba alimsogelea mama huku mkono wake wa kulia umeshika mkanda wa suruali yake. Mama akiwa uchi wa mnyama, amejikunja chini kwa uoga kama kifaranga. Mama Hamis naye amekaba shingo yangu; kunizuia nisiokoe maisha ya mama yangu. Mdogo wangu Shadrack yupo pembeni ya mama analia kama yatima. Bila huruma, bila kujali baba aliinua mkono wake wenye mkanda na kuanza kumsulubu mama mbele ya macho yetu. Mbele ya hawala yake.

Tuesday, June 24, 2014

Nikumbuke Mpenzi wangu part 2

Mungu nimekosa nini. Mungu nisaidie.....Nikasikia sauti ya madaktari wakipumua kwa furaha. Michael akasema; "Dokta...umemrudisha". Wote kwa pamoja wakafurahi. Dokta Adam alionyesha kufurahi zaidi. Sauti yake ya furaha; ilipenya ndani ya masikio yangu. Hii ilinipa amani; nikajua labda nimerudi. Wote wakavua glovu na kuzitupia ndani ya chombo cha kuutupia uchafu. Niliwasikia kwa makini sana, nilitaka kujua ni kitu gani kinaendelea. Baada ya dakika kadhaa nikasikia sauti ya Debora.

Friday, June 20, 2014

MAISHA YANGU DUNIANI PART 1: MAHOJIANO KATI YA MUNGU NA MWANADAMU

MAISHA YANGU DUNIANI PART 1: KILA IJUMAA.
Ilikuwa tarehe 12/06/1982, siku nilipokufa na kuondoka duniani. Ni siku niliyokutana na Mungu uso kwa uso, katika ulimwengu mwingine, unaofahamika kwa majina mengi; wengine huita mbinguni, wengine Ahera, kulingana na imani tofauti. Nikiwa nimebeba mizigo yangu ya ndoto nilizoshindwa kuzifikia duniani, mawazo niliyoogopa kuyatoa, vipaji na zawadi nilizopewa na Mungu nivitumie;
Nilipofika geti la mbinguni; nilikutana na malaika. Nilisalimia; kwa heshima. Na kujibiwa;
"Hiyo mizigo ya ndoto zako,vipaji na zawadi za maisha hairuhusiwi  kuingia nayo mbinguni. Mungu alikupa ili itumike duniani na siyo mbinguni. Kwani wewe ulikuwa unafanya nini duniani miaka 89 yote iliyopita? Umekufa ukiwa na miaka 89, hujatumia hata kitu kimoja? Hapana; huwezi kuingia. Ondoka hapa"

Thursday, June 19, 2014

"Siri Inayoangamiza" :The Secret that kills: Part One...........REVISED


"Siri Inayoangamiza"  Part One...........REVISED
"Maisha yako yapo salama, kwasababu huijui siri. Lakini kutokuijua siri; huyajui maisha. Na kamwe hutaujua utamu wa maisha"  -SIRI INAYOANGAMIZA

Ilikuwa tarehe 31/12/2000 siku ya Jumapili muda wa saa sita na nusu usiku,  Steven  Mtambaji  muigizaji maarufu wa filamu za kitanzania akiwa amelala katika chumba chake  mbezi beach – Dar Es Salaam. Alisikia sauti ya kike ikiita "Steve…Steve...nifungulie".  Alishtuka kutoka usingizini. Na kwenda kufungua mlango.

Wednesday, June 18, 2014

NILIOLEWA NA KAKA YANGU: I married my blood brother part 1.



NILIOLEWA NA KAKA YANGU: Based on a true story KILA JUMATANO. 
Nikasikia sauti kutoka moyoni  mwangu ikiniambia “Tulia moyo wangu. Tulia mwanangu haya yote yatapita. Haya yote yataisha. Ipo siku, ipo siku dunia yako itabadilika”.
Niliposikia sauti hiyo nilifuta machozi na kukificha kisu, ambacho kama siyo sauti hiyo ningemchoma baba yangu mzazi tumboni. Nilikaaa chini kuyasikilizia maumivu.  Baba yangu hakuonyesha kujali; aliendelea kumpiga mateke mama yangu. Nilishindwa kuyavumilia, ndiyo nilishindwa kuyavumilia nilimsogelea na kumchoma mapaja yake.Kwasababu sikutumia nguvu kutokana na uoga; sikumuumiza. Alinigeukia na kunikanyaga bila huruma bila kujali kuwa mimi ni mtoto wa miaka nane. Mama akapiga kelele; 

Tuesday, June 17, 2014

Nikumbuke Mpenzi wangu:Remember me my love Part 1






“Dokta Adam….Dokta Adam hatutaweza kumrudisha mgonjwa  huyu. Lazima tutampoteza”
Ilikuwa ni sauti ya mwanamke niliyoisikia kwa mbali. Nilijaribu kufanya  kila ninachoweza lakini mwili wangu haukuwa na uwezo tena.  Sikujua nipo wapi na kwanini. Macho yangu hayakuwa na uwezo wa kuona. Pua yangu; haikuweza kuambulia harufu yoyote.

Nilianza kujiuliza kuhusu  sauti  ya mwanamke iliyosikika kupitia masikio yangu ikisema Dokta Adam hatutaweza kumrudisha mgonjwa huyu. Lazima tutampoteza. Nilijiuliza mgonjwa huyo ni nani? Je ni mimi au ni mtu mwingine? Na hapa nipo wapi? Nimefikaje?Wakati bado najiuliza maswali yasiyo na majibu nikasikia sauti ya kiume ikisema:
“Patricia..Patricia huwezi kufia katika mikono yangu. Mateso uliyoyapata kwasasa yanatosha. Huwezi kufa. Huwezi kufia ndani ya chumba changu cha operesheni. Huwezi kufa… amka….amka Patricia”